Home » , , » UNATAFUTA AJIRA? MBINU RAHISI ZA KUSHINDA USAILI WA KWENYE SIMU…

UNATAFUTA AJIRA? MBINU RAHISI ZA KUSHINDA USAILI WA KWENYE SIMU…

Written By Unknown on Sunday, August 31, 2014 | 11:08 PM


1. Fanya utafiti wa kutosha kuhusu shirika,Hii itakusaidia kujibu maswali kwa wepesi.
2. Jiandae kwa maswali ya usaili wa simu,hakikisha unayasoma maswali ya msingi katika usaili wa simu na upate majibu mapema kabla ya usaili
3. Tumia simu ya mezani/simu ya mkononi yenye mawasliano ya uhakika,Ili kuepuka simu kukatika wakati wa usaili.
4. Zima muito wa kusubilisha(Turn off call waiting) Hii itaondoa usumbufu wa kupigiwa simu wakati unaongea na itakutoa katika ufanisi wa usaili.

5. Kaa sehemu yenye utulivu,Epuka kukaa kwenye kelele ya vitu na watu mbalimbali kama vile mashine au hata watoto wadogo
6. Uwe na gilasi ya maji,hii itakusaidia kulainisha koo wakati unaoongea na utakunywa kwa haraka na kuendelea na mazungumzo
7. Chukua kumbukumbu, ni vema ukaandika baadhi ya mambo ya msingi ili iwe kumbukumbu kwa baadae itakapohitajika.
8.Sikiliza kwa umakini,Ni vema ukasikiliza ili kuulewa kile kinachoulizwa na  uweze kujibu na kama hujaelewa ni vema ukauliza ufafanuzi zaidi.Kumbuka kuchukua sekunde kadhaa kabla ya kujibu ili kuweza kuyaweka mawazo yako pamoja kwa ufanisi, usiharakishe kujibu.

9. Andaa maswali ya kuuliza mapema,Pale utapopewa fursa ya kuuliza hakikisha uko tayari na maswali yako.

          ………..Maktaba YETU leo……….
. “Strength does not come from winning. Your struggles develop your strengths. When you go through hardship and decide not to surrender, that is strength”
 Arnold Schwarzenegger
Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi