Home » » Usaili..majibu ambayo kila mwajiri huyategemea kutoka kwa anayeomba kazi..ndo haya

Usaili..majibu ambayo kila mwajiri huyategemea kutoka kwa anayeomba kazi..ndo haya

Written By Unknown on Thursday, August 28, 2014 | 4:28 AM

 

Unapokwenda katika usaili ni wazi kwamba unakuwa umejiandaa kujibu maswali kadhaa kutoka kwa mwajiri.Jambo moja la kuzingatia ni kwamba mwajiri kuna majibu anayotegemea kutoka kwako kwa kipindi chote cha usaili ambayo ndo hasa msingi wa usaili.Haya ndo majibu husika soma…

1.Je unao ujuzi wa kufanya kazi?
Siku zote mwajiri jambo la kwanza analotaka kulitambua kutoka kwako ni kuona kama unao ujuzi wa kazi husika mfano,unaomba nafasi ya afisa masoko.Mwajiri ataangalia ujuzi ulonao katika nafasi hiyo kulingana na uzoefu mbalimbali.Pia ataangalia ni maarifa gani utahitaji kupitia mafunzo mbalimbali kazini ili uwe katika ubora zaidi.
2. Je unaendana na nafasi husika
Kila shirika linatamani kuona namna gani unaweza kufanyakazi katika idara husika kwa ufanisi wa hali ya juu.Lakini pia mwajiri anatazama ni kwa vipi unaweza kufanyakazi na watumishi wenzako na kuwa msaada katika kuwasaidia kuendeleza vipaji vyao katika kazi.
3. Je unalifahamu shirika na nini linachofanya?
Kama shirika linafanya kazi ambazo zinaendana sawa na taaluma yako ni wazi kwamba utavutiwa kufanya kazi katika shirika hilo.Waajiri wengi wanapenda kusikia majibu ambayo yanaonesha wazi kuwa wewe hujaomba kazi kwa vile huna kazi au unataka mshahara ila umeomba kazi kwa vile unapenda kufanya kazi katika shirika hilo.
4. Je unawezaje kukabiliana na washindani wenzako?
Unapoenda katika usaili unalinganishwa na wale ambao pia wameeomba nafasi hiyo,hivyo siku zote mwajiri anapenda kuona wewe utafanya usaili kwa kiasi gani ili kuweza kuwashinda wenzio.Hivyo zingatia maandalizi na pia ujue mbinu mbalimbali kwa kusoma na kutembelea blog mbalimbali ikiwa ni pamoja na blog hii ya Amewezaje.

5. Je unahitaji kazi uloomba?
Waajiri wengi wanatambua kwamba wale wanaoomba nafasi za kazi ni dhairi wanahitaji kazi hizo.Utofauti unakuja pale ambapo wengine wanapofanya maandalizi ya kutosha kuhusu usaili na wengine wanaenda pasipo kuzingatia haya.Jambo la msingi hapa jitahidi kuthibitisha kuwa unahitaji kazi hiyo kwa kuwa na majibu mazuri ya uhakika.


………..Maktaba YETU leo……….
“If you fulfill the wishes of your employees, the employees will fulfill your visions.”
    Amit Kalantri


Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi