Home » » Hizi ndo sentensi tatu zitazofanya barua yako isichaguliwe kwenye usaili

Hizi ndo sentensi tatu zitazofanya barua yako isichaguliwe kwenye usaili

Written By Unknown on Thursday, August 28, 2014 | 7:14 AM


Utafiti wa wataalum mbalimbali unaonesha watu wengi wanaandika barua za kazi kama daraja la kumwelekeza mwajiri asome "CV" zao,kosa hili linawagharimu kila uchao kwani mwajiri asipovutiwa na barua hawezi kusoma "CV" bali huweka pembeni na kusoma za wengine.Zingatia hizi hatua tatu ili utoke katika wimbi hilo

1. Andaa barua ya  kielelezo(Creat a cover letter Template)
Katika barua hii  andika taarifa zote za msingi zinazotakiwa katika barua kama vile ujuzi pamoja na uzoefu ulonao.Kisha hifadhi barua hiyo kwenye kompyuta yako au vinginevyo ambapo ni rahisi kuiona.

2. Binafsisha barua yako(Personalize Your Cover Letter)
Kila wakati utapataka kuomba kazi fungua kielelezo na tengeneza nakala nyingine kisha anza kubadili taarifa zilizopo ili ziendane na sehemu unayotuma maombi.
·    Badili anwani,ili uandike anwani ya mwajiri unayemtumia
·        Badili Cheo/salaam za awali cha/za Yule unayemtumia,andika jina lake kama unalifahamu mfano “Dear Ms Jones” "Human Resource Manager"
·  Badili aya ya kwanza,ili kueleza nafasi unayoomba na ulipoona tangazo husika.
Badili kiini cha barua,kwa kuandika ujuzi na uzoefu unaohitajika kulingana mchanganuo wa kazi husika
 Aya yako ya mwisho pamoja na sahihi havina haja ya kubadilishwa
· Hakikisha unahifadhi kila barua unayotuma ili kukusaidia katika kumbukumbu
Njia hii ni rahisi sana kuliko kuanza kuandika barua mwanzo na pengine uko na muda mfupi sana ni rahisi kusahau mambo mengi ya msingi.Hii itakufanya kuepuka kuandika barua isiyonamvuto inyosema “Tazama CV yangu”
3. Hakiki barua yako kabla ya kuituma
Hii itakusaidia kubaini makosa madogo madogo kama ya herufi na sarufi ambapo ukituma hivyo yataweza kukugharimu.
………..Maktaba YETU leo……….

 There's only one interview technique that matters... Do your homework so you can listen to the answers and react to them and ask follow-ups. Do your homework, prepare.
Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi