Home » » Hili si swali la kukosea tena katika interview..tazama majibu yake

Hili si swali la kukosea tena katika interview..tazama majibu yake

Written By Unknown on Tuesday, August 19, 2014 | 11:48 AM












What is your greatest strength?


Ni dhairi kwamba suala la ajira katika ulimwengu wa leo ni la ushindani wa hali ya juu na hivyo kama hautakuwa makini itakuchukua muda mrefu sana kupata ajira iwe serikalini au katika mashirika au taasisi zisizokuwa za kiserikali kwani kila mwajiri anataka mtu bora atayeweza kufanyakazi kwa ufanisi wa hali ya juu.Kipimo muhimu katika hilo ni namna utavyoweza kujielaza katika usahili.Unaweza kusoma miaka mingi katika taaluma yako lakini ukashindwa kuelewa kuwa usahili pia ni taaluma.Ukumbuke kuwa hata kuitwa katika usahili ni jambo la bahati sana sasa, kwa nini usitumie fursa hiyo kupata hiyo ajira kwa sababu wamekuona unafaa tayari, kilichobaki ni wewe kwenda kuthibitisha umahiri wako.
Leo nakupatia mbinu thabiti ambazo wengi wamezitumia katika kuijbu swali hili na kupata ajira bila pingamizi.Kumbuka kwamba wakati wa usahili wale wanaokusaili(Interviewers) wanakuwa makini sana katika swali hili kuhusu uwezo wako(your strength) ambapo itaonesha wazi ni jinsi gani unauwezo katika kazi hiyo.

"What is your greatest strength?"(ni nini uwezo wako) hili ni miongoni mwa maswali rahisi sana katika interview ingawa wengi wamekuwa wakishindwa kulijibu.Unapoulizwa swali hili kuhusu uwezo wako jambo kubwa hapa ni kuzingatia sifa ulizonazo ambazo zitakufanya ufuzu katika nafasi hiyo.
Njia rahisi ni wewe kuelezea ujuzi na uzoefu ulonao ambao moja kwa moja unaendana na nafasi uloomba.Napozungumzia uzoefu na ujuzi si maanishi tu kwamba lazima ulikuwa umeajiriwa unawezakuwa umepata uzoefu na ujuzi hata kutoka shuleni,kujitolea n.k

MAMBO MATATU YA KUZINGATIA.

11.    Hakikisha umesoma mchanganuo wa kazi(job description) ili uje nini kinahitajika katika nafasi hiyo.Baadhi ya matangazo kazi uorodheshe sifa zinazohitajika wakati wengine huwa hawaweki sifa hizo.Hivyo, unahitaji kukusanya maelezo ya ziada kabla hujaenda katika usaili. Unaweza kutafuta taarifa kwa, tovuti au kwa mwajiri mwenyewe pale inapohitajika hii itakusaidia kutambua ni wapi ujikite katika kuelezea uwezo wako(Strength) kulingana na mahitaji husika.

2 2. Tengeneza orodha maeneo ulio na ujuzi nayo kulingana na hitaji la nafasi husika.unaweza kuorodhesha sifa nyingi tu na ujuzi huo wawezakuwa katika elimu,uzoefu wa kazi ,ujuzi binafsi.Hii itakusaidia kumfanya mwajiri wako atambue kuwa unaujuzi ambao utasaidia kufanikisha mafanikio ya kazi husika,badala ya kusema tu kuwa unaujuzi pasipo kutaja ni kwa namna gani umewezapata ujuzi huo.kumbuka kutoa mifano ni kwa jinsi gani ulitumia ujuzi huo katika kukabiliana na mambo hadi ukafanikiwa maneno matupu bila mifano katika interview hayana mashiko kabisa.

   3. Andaa hadithi fupi.
Njia nyigine ni kuandaa hadithi  ambayo unaeleza  namna ulivyotumia uwezo wako katika kufanikisha tukio Fulani ambalo lilko sawa na nafasi uliyoomba. Matukio haya lazima lifute utaratibu ambapo unaweza unaweza kuelezea hali au changamoto; na hatua  ulizochukua; na matokeo, uwezo ulopata  au athari za ushiriki wako.lengo mahususi hapa lazima kuonesha uwezo ulionao ambao unaweza kuutumia pia katika nafasi unyoomba.

Tazama mifano ya majibu ya swali hili na imeandikwa kwa lugha ya kiingereza ambapo utaipata kwa ufasaha zaidi.

“I have exceeded my sales goals every quarter and I've earned a   bonus each year since I started with my current employer.”
“My time management skills are excellent and I'm organized, efficient, and take pride in excelling at my work.”

“I pride myself on my customer service skills and my ability to resolve what could be difficult situations.”
Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi