Home » , , , , , » UNATAFUTA AJIRA..WENGI HAWAFAMU MBINU NYEPESI YA KUAJIRIWA..SOMA SENTENI HIZI

UNATAFUTA AJIRA..WENGI HAWAFAMU MBINU NYEPESI YA KUAJIRIWA..SOMA SENTENI HIZI

Written By Unknown on Tuesday, August 26, 2014 | 1:05 AM


Ni dhairi kwamba suala la ajira kwa hivi sasa ni changamoto kubwa sana,na hivyo pasipokuwa na mbinu mbadala huwezi kupata ajira kirahisi kwa kipindi kirefu,utafiti unaonesha kuwa wengi wa wahitimu wanazunguka na bahasha kila uchao pasipo mafanikio na miongoni mwa sababu kubwa hawana uzoefu wa kutosha.Blog yako ya Amewezaje inakuletea mbinu rahisi ya kupata kazi,na mbinu hiyo ni kufanya kazi ya kujitolea Kuna faida nyingi sana katika kufanya kazi ya kujitolea ni wazi kuwa hata wewe umeshuhudia watu wakipta ajira kwa njia hii.Leo nakupa faida kuu nne za kufanyakazi kwa kujitolea(Internship/volunteer)


1. Unapata fursa ya kuandika uzoefu wako katika ‘CV’ yako.Hii itakutengenezea wigo mkubwa wa kupata kazi kwani unaonesha tayari unafahamu jinsi ya kufanyakazi.

2. Unapata uzoefu unaotakiwa katika kazi.Waajira mara nyingi wanaangalia uzoefu wa jumla ambao hata wakikuajiri unawezaanza kazi mara moja.

3. Kujua kwa undani zaidi kuhusu kazi.Hii ni pamoja na kupata mbinu mbalimbali za kazi ikiwa ni pamoja na kukabiliana na changamoto zinapokuwa zinajitokeza katika kazi.

4.Kutengeneza mtandao na watu mbalimbali.kumbuka kuwa kufahamiana na watu ni mtaji mkubwa sana katka maisha hivyo ni rahisi sana kupata kazi.Jitahidi kuwa na mawasiliano ya watu wengi wanaoweza kukupa habari mara kwa mara.

………..Maktaba YETU leo……….
. “Do not hire a man who does your work for money, but him who does it for the love of it.”

   Henry David Thoreau, Life without Principle
Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi