Home » , » Haya ndo majibu yanayofaa unapokwenda kwenye usaili kutokea kazini(unapotaka kubadili kazi)

Haya ndo majibu yanayofaa unapokwenda kwenye usaili kutokea kazini(unapotaka kubadili kazi)

Written By Unknown on Thursday, September 11, 2014 | 8:38 AM










Swali,…Kwanini umeacha kazi ulokuwa unafanya?

Swali hili mara nyingi linakuwa na majibu mbalimbali lakini inategemea na kazi unayoomba pamoja na mazingira.Blog yako ya Amewezaje baada ya utafiti kutoka kwa wataalamu mbalimbali wa mambo ya ajira inakuletea mfululizo wa majibu ambayo unaweza kutumia kujibu swali hili.


a.Nilijiuzulu kwa sababu katika kazi nilokuwa nafanya kulikuwa hakuna fursa ya kutosha kwa mimi kuendelea katika maneo ya taaluma yangu.

b.Nilipotoka katika masomo niliamua kutafuta kazi nyingine kwasababu nilitaka kupata uzoefu tofauti kulingana na taaluma niloisomea katika chuo.

c.Kusema kweli nafasi nilokuwa nikiitumikia haikuwa inaendana na taaluma yangu,hivyo nikaona ni vema nijiuzulu katika nafasi hiyo.

d.Kazi nilokuwa nafanya ilikuwa ya muda hivyo nikaamua kujiuzulu ili nitafute kazi ya mkataba wa muda mrefu.

e.Niliamua kujiuzulu ili niweze kujifunza changamoto mpya na kujifunza mambo mapya tofauti na nilojifunza katika kazi yangu ya awali.


f.Familia yangu ilibadirisha makazi na kuhamia eneo jipya  na katika eneo hili hakuna ofisi za shirika nilokuwa nafanya kazi,hivyo niliamua kujiuzulu.





Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi