Home » » HAYA NDO MAKOSA MADOGO MADOGO LAKINI YANAWAGHARIMU WENGI KATIKA USAILI (INTERVIEW)

HAYA NDO MAKOSA MADOGO MADOGO LAKINI YANAWAGHARIMU WENGI KATIKA USAILI (INTERVIEW)

Written By Unknown on Sunday, September 7, 2014 | 9:28 AM


Mpendwa msomaji siku zote tunasema kuwa suala la usaili linahitaji umakini wa hali ya juu sana na hivyo ni vema ukazingatia kila kipengele unachofanya ili kujihakikishia nafasi unayoomba.Leo blog yako ya Amewezaje inakuonesha makosa ambayo ni madogo laikini yananafasi kubwa sana katika usaili…

1. Kuchelewa kufika katika usaili-Hapa itakufanya kutokupata muda wa kutafakari na kupangilia mambo yako,pia mwajiri atapoteza imani nawewe kuwa hata wakati utakapoajiriwa waweza kuwa unachelewa maana jambo hili kwako ni la kawaida(Tabia)
2. Kutokuzima simu –si rahisi kufahamu ni wakati gani unawezakupigiwa simu wengi wamepigiwa simu wakiwa katika usaili na matokeo yake wamepoteza mwelekeo kabisa na hata kukosa nafasi husika.Unaweza kuzima simu au kuundoa sauti na hata kuweka mtetemo iwapo unaulazima wa kufanya hivyo.Vinginevyo zima simu ili kuiweka akili yako katika usaili kwa asilimia 100%
3. Kujibu swali pasipo kulielewa-Wengi hukimbilia kujibu maswali wakati hawajaelewa na matokeo yake wanajibu isivyosahihi.Siku zote jitahidi kulielewa swali kama hujaelewa ni vema ukauliza kueleweshwa ili upate kujibu kwa ufasaha zaidi
4. Kutokuzigatia lugha ya mwili-Katika usaili lugha ya mwili ni jambo la msingi sana ambapo ni muhimu kunzigatia.Maelezo zaidi tembelea blog hii katika matoleo yake ya awali upate kusoma zaidi.
6. Kuvaa chini zaidi au juu zaidi ya  unavyovaa mara nyingi-Ukivaa chini au juu zaidi ni dhairi utakuwa katika hali ambayo si ya kawaida na kukufanya muda mwingi kufikiri juu ya mavazi maana si halisi.Zingatia kuvaa katika kiwango cha wastani pia zingatia aina ya kazi unayoomba.
7. Kutokushukuru-Ni vema baada ya usaili ukashukuru kwa njia utayoona inafaa ingawa njia bora ni kwa barua pepe au barua ya kawaida.Kushukuru sio mpaka uwe umechaguliwa tu pia kuitwa katika usaili ni jambo la kuwashukuru kwa kukuona unafaa.

8. Kusalimia bila kujiamini-Usaili unaanza pale tu unapoonana na mwajiri wengi wamekuwa na wasiwasi sana wakati wanaposhikana mkono kwa salamu.Zingatia unaposalimiana na mwajiri toa sauti ya uhakika na umtazame usoni na kumuuliza jambo moja au mawili.
………..Maktaba YETU leo……….
. “Strength does not come from winning. Your struggles develop your strengths. When you go through hardship and decide not to surrender, that is strength”
 Arnold Schwarzenegger
Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi