Wengi wanaotafuta
kazi wameonekana kupuuzia kuandika barua za kikazi kwa kuamini kuwa “ CV” zao
ndo muhimu hilo ni kosa kubwa sana na wengi wamepoteza nafasi ya kwa njia
hiyo.Hapa Blog yako ya Amewezaje kwa utafiti wa muda mrefu inakuonesha makosa
ambayo wengi wanayafanya katika kuandika barua za maombi ya kazi..
1.Kutuma barua yenye
makosa madogomadogo.mfano makosa ya kisarufi na herufi hii ni tatizo kubwa
kwani mwajiri anaona wewe hauko makini hivyo barua yako utupiliwa mbali.Pitia
barua yako kabla hujaituma.
2.Kutuma barua ya jumla(barua moja
inatumwa kwa watu waajiri wengi bila
kurekebishwa)Hakikisha unataja kazi unayoomba kwenye sentensi ya kwanza.Elezea
uzoefu wako na ujuzi wako kulingana na nafasi husika.
3.Barua kutokwenda kwa mhusika.Wengi wa
wanaoomba kazi wametokea kutuma barua kwa mtu ambaye si sahihi hii ni kutokana
na kutuma maombi mengi ya kazi.Hakikisha unapitia mawasiliano yako kabla
hujatuma kwa mhusika.
4.Kutumia salamu zilizopitwa na wakati.Wengi
hutumia salamu za zamani sana kama vile “Dear Sir or Madam” Unaweza tumia “Dear
Human Resource Manager”Kama unamfahamu waweza
andika jina lake mfano kwa mwanamke tumia “Ms. Rachel” badala ya “Mrs
Rachel”
5. Barua kuwa fupi sana.Barua kuwa fupi ni
hali itayopelekea mwajiri kuona kuwa nia yako
ni ndogo sana katika kazi.Pia hutashindwa kueleza uzoefu wako na
historia katika kazi ulokuwa ukifanya na hivyo huwezi kumshawishi mwajiri kwa
lolote.
6.Barua kuwa ndefu sana.Barua ikiwa ndefu
zaidi inawezakuwa mzigo kwa msomaji na inamshawishi kuiacha na kusoma za watu wengine.Hakuna
haja ya kuwa na aya nyingi katika barua aya 3 hadi 5 zinatosha sana na zisiwe
na mistari zaidi ya 6.
7.Kuandika barua yenye maelezo mengi yasiyo
lazima.Kuna taarifa ambazo si za kundikwa kwenye barua,unatakiwa kuandika
taarifa zinazohitajika katika nafasi husika kwa mwajiri.Barua ikiwa ndefu itakupunguzia
uwezekano wakuchaguliwa katika usaili.
8.Kutokutoa mifano halisi.Kueleza mawazo
matupu kuhusu uwezo wako pasipo mifano ya majukumu ulofanya ambayo yamekupatia
uwezo huo ni kazi bure na huwezi kumshawishi mwajiri.Taja mifano hai na
majukumu ulokuwa ukifanya yalokupa ujuzi mfano ninauwezo mkubwa wa mauzo kwani
kwa kipindi nilichofanya kazi katika kampuni x nimewezesha kampuni kuuza mara
tatu ya mauzo ya kawaida.
………..Maktaba YETU leo……….
“Time spent on hiring is time well spent.”
“Time spent on hiring is time well spent.”
Robert Half
Post a Comment