Home » » SIRI NZITO NDANI YA CHUMBA CHA USAILI(INTERVIEW)

SIRI NZITO NDANI YA CHUMBA CHA USAILI(INTERVIEW)

Written By Unknown on Friday, August 22, 2014 | 6:38 AM


Unapokwenda kwenye usaili ni wakati muafaka kwa mwajiri kuonana nawewe na kupenda kufahamu mambo kadhaa kutoka kwako,kama vile uwezo wako wa kukabiliana na mamba,utu wako na kwa vipi unaweza kufanya kazi katika shinikizo(pressure)Kwahiyo ni muda mzuri kwako kuonesha ubora wako kimasoko na hii itamfanya mwajiri aone sabababu ya kukuajiri.Tatizo kubwa ni kwamba unakwenda kwenye usaili pasipo kupata habari za taasisi au shirika husika kwa kufahamu malengo ambapo ndo dira ya shirika hilo.Siku hizi mashirika mengi yanaweka taarifa zao katika mitandao tafadhali soma kwa kina ili upate mwanga katika kujibu swali hili.

SWALI:kwanini unataka tukuajiri?(Why should we hire you?)

Swali hili mara nyingi huwezi likwepa na wengi wamepoteza nafasi kwa kukosea majibu.Hakuna kulikosa tena.Zingatia haya mambo manne kwenye majibu yako.unapojibu usiwe na wasiwasi jibu kwa utulivu na kwa kufurahi.

1. Tambua ujuzi unaohitajika katika nafasi hiyo(Skills needed for the job)-Ukieleza usieleze ujuzi nje ya unohitajika….

2. Tambua malengo ya nafasi hiyo(Goals for the position)-Jieleze ukilenga utafanyanini au unanini kitachochangia malengo hayo kutimia.

3. Historia yako katika kazi na elimu(Job background)-Katika hayo maelezo zingatia uzoefu ambao kwa kiasi kikubwa unashabiliana na kazi unayoomba sio kueleza kila kitu.

4. Zingatia kusoma vizuri mchanganuo wa kazi kwani huwezi kuoanisha maelezo yako kama hujasoma huo mchanganuo(Job description)

Soma mifano hii kwa maarifa zaidi si kwamba lazima uitumie kama ilivyo.

Kwanini unataka tukuajiri?

Katika nafasi hii ya (…JAZA….) katika kampuni hii kwangu mimi ni nafasi sahihi sana.Nina shahada ya (…JAZA……),nina uzoefu na maarifa nilivyovipata katika kazi nilokuwa ninifanya katika Kampuni (…TY.).Nina uwezo mkubwa wa kufanya kazi kwa maadili,na ni mtu wa kutegemewa kaitka kazi kwani kwa bidii yangu nataraji kufanyakazi kwa kiwango cha juu.

Kwanini unataka tukuajiri?
Iwapo ninapata fursa hii, ninatajitahidi kuhakikisha kampuni(XY….)  inaongeza faida na kufikia malengo yake.Nina elimu ya kutosha,ninauwezo wa kufanya kazi kama kiungo muhimu pia napenda kujifunza vitu mbalimbali katika kazi ili kuleta ufanisi.Hii nafasi ninaitazamia sana na iwapo nitaipata nitakuwa hazina kubwa katika shirika hili.

Kwanini unataka tukuajiri?
"Najisikia kuwa mimi ni mtu sahihi kwa nafasi hii kwa sababu ya uzoefu wangu, haiba(personalty) yangu, na elimu yangu. Nina dhamira na ujuzi muhimu kwa ajili ya kazi hii.kumbukumbu za kazi zitakudhirishia kwamba mimi ni mtu wa kutegemewa, mfanyakazi ngumu , na naweza kufanya kazi pamoja.Nimevutiwa sana na kampuni hii ya(…CV.. ) na ntajisikia upendeleo kufanya kazi hapa. "
   
………..Maktaba YETU leo……….
“You can’t teach employees to smile. They have to smile before you hire them.”
 Arte NathanWynn Las Vegas


Share this article :

+ comments + 1 comments

August 24, 2014 at 10:14 AM

Uko vizuri kijana, komaa

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi