Home » » Maeneo 3 ya lazima ambayo wengi hawafanyi utafiti kabla ya kwenda katika usaili..Soma hapa

Maeneo 3 ya lazima ambayo wengi hawafanyi utafiti kabla ya kwenda katika usaili..Soma hapa

Written By Unknown on Friday, September 12, 2014 | 1:53 AM


Kabla ya kwenda katika usaili ni vema ukakusanya taarifa za  kutosha ambazo zitakusaidia sana katika kupata nafasi uloomba.Utafiti huu umeganyika katika makundi makuu matatu kama ifuatavyo

1. Jitafiti wewe mwenyewe(you)-katika utafiti huu unatakiwa kujiuliza maswali yafuatayo na kupata majibu yake kabla ya kwenda katika usaili
-Je nina uwezo wa kufanya kazi hiyo?
-Nitawezaje kutimiza malengo ya mwajiri wangu?

2. Fanya utafiti kuhusu nafasi husika(position)-katika sehemu hii ni vema kuelewa kwa kina nafasi unayoomba ili kuwa katika mazingira mazuri ya kujibu maswali yanoyoelekezwa kwenye eneo husika, hakikisha unafahamu haya:-
-Elewa hitaji na majukumu ya nafasi husika
-Zingatia vipengele vyote vya nafasi hiyo na kuvitathimini kwa kina.

3. Fanya utafiti kuhusu mwajiri wako pamoja na shirika(Employer & Company)-ni vema ukafahamu mambo kadhaa kabla ya kwenda katika usaili ili kuwa katika nafasi nzuri ya  kujibu maswali,hivyo ni vema kuzingatia haya:-
-Historia ya shirika husika
-Shughuli zote zinazofanywa na shirika husika

-Mfumo mzima wa uongozi/utawala wa shirika husika pamoja na idara zake zote.
Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi