Home » , » Mambo 2 ya kuzingatia baada ya usaili(Interview)

Mambo 2 ya kuzingatia baada ya usaili(Interview)

Written By Unknown on Monday, October 27, 2014 | 10:24 AM


Mpendwa  msomaji mara tu baada ya kumaliza usaili si kwamba utakuwa umekamilisha majukumu yako yote kwani bado kuna mambo ya msingi unayotakiwa kufanya.Hapa kuna mambo makuu mawili ya kufanya mara baada ya usaili.


Uliza kama kuna hatua nyingine ya usaili.Katika usaili kila taasisi inakuwa na utaratibu wake wa kufanya usaili hadi kuajiri,baadhi ya mashirika hufanya usaili kwa njia tofauti tofauti mfano: Usaili wa kuandika(Written) mahojiano (Oral),kwa njia ya simu(Phone interview) n.k.Jambo la kuzingatia hapa ni kwamba si taasisi zote zinaweza kufanya yote kwa wakati mmoja lakini pia zinawezakufanya kwa wakati mmoja na kurudia ili kufanya mchujo wa kupunguza idadi ya wasailiwa.Hivyo basi ni vema ukawa na taarifa za kutosha kuhusu hatua za usaili zinazofuata ili upate muda wa kujiandaa.Unaweza kuuliza pindi tu unapopata fursa ya kuuliza katika chumba cha usaili ama baada ya usaili.


Tuma barua ya shukrani.Shukrani  ni miongoni mwa mambo ya msingi ambayo mwanadamu hupenda kutendewa,hivyo hata katika usaili suala hili lina uzito sawa.Ni vema ukatuma barua fupi yenye sentensi chache za kushukuru kwa fursa na thamani kubwa ulopewa na taasisi kuitwa katika usaili.Unaweza kuandika barua pepe(Email)yenye maneno mafupi ya shukrani .Kumbuka ni vema ukaandika barua ndani ya masaa 24 mara baada ya usaili,kama huwezi kupata fursa ya kuandika barua mara baada ya usaili unaweza kuandaa na baada ya usaili ukaikabidhi kwa wahusika.Wengi  hawafanyi suala hili lakini lina nafasi kubwa ingawa baadhi ya taasisi hawalipi suala hili uzito.
Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi