Home » » Haya ndo maswali unayotakiwa kuuliza katika interview pindi unapopewa fursa………….

Haya ndo maswali unayotakiwa kuuliza katika interview pindi unapopewa fursa………….

Written By Unknown on Wednesday, August 20, 2014 | 2:57 PM



Ni utaratibu uliopo mara baada ya kujibu maswali wakati wa usaili (interview) unapewa fursa  kuuliza maswali.Katika eneo hili ndipo wengi hushindwa kujua ni nini cha kuuliza.Blog yako ya Amewezaje inakuletea mbinu nyepesi za nini cha kuuliza unapopewa fursa hii. Zingatia haya:


Hakikisha unauliza maswali ambayo yataonesha kwa namna gani utaweza kukizi mahitaji ya mwajiri wako.Mfano unawezauliza mradi au shughuli mahususi utakazojihusisha nazo pindi watakapokuajiri.Hii itaonesha jinsi gani unadhamira ya dhati katika kufanya kazi  na kuleta tija usiweke maslahi yako mbele kuliko ya mwajiri.

Unaweza kuhuliza maswali kulingana na taarifa zaidi unazofahamu kuhusu shirika hii pia itakuongzea alama nyingi kwa kuwa utauliza vitu kwa kina zaidi.
Iwapo hutaambiwa tarehe ya kupata majibu na namna utavyotaarifiwa ni muhimu kuuliza swali hilo.Wengi husema majibu ni ndani ya siku kadhaa na ukiona hujataarifiwa ujue hujachaguliwa kama hawajatoa taarifa hiyo ni vizuri ukachukua hatua ya kufuatilia.Katika mada zinazokuja tutalizungumzia hili kwa kina.

Usiulize kuhusu mshahara au maslahi mengine kama posho kwa ujumla usiulize mwajiri atakufanyia nini.Maswali haya yatakuonesha kuwa unatanguliza ubinafisi na sio kazi kwa ufupi umefuata pesa sio kazi.Si kwamba hupaswi kujua taarifa hizo lakini pale si mahali sahihi pa kuuliza.Katika mada zetu tutakuonesha ni wapi pa kuuliza.

………..Maktaba YETU leo……….
. “The key for us, number one, has always been hiring very smart people.”

 Bill Gates, Microsoft
Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi