Home » » Maswali 3 ambayo hutakiwi kumuuliza mwajiri wakati wa usaili

Maswali 3 ambayo hutakiwi kumuuliza mwajiri wakati wa usaili

Written By Unknown on Monday, September 1, 2014 | 12:00 AM


Wakati wa usaili ni wakati muhimu na hadimu sana,hivyo unahitaji umakini wa hali ya juu zaidi katika matumizi yake.Baadhi ya maswali unaweza kuyauliza  kumbe ndo inakuwa safari yako ya kupoteza ajira.Hivyo maswali mengine ni ya kufanya utafiti na mengine ni ya kumuuliza mwajiri mara baada ya kupata fursa unayoomba.Yafuatayo si maswali ya kuuliza katika usaili…


1. Mtanipa mshahara kiasi gani?Swali hili si sahihi wakati wa usaili sababu kubwa ni kwamba suala la mshahara litakuja mara baada ya kuchaguliwa katika nafasi husika kutokana na uwezo wako katika usaili.Pia ni vema ukafanya utafiti kuhusu mshahara mapema ili uje viwango kulingana na nafasi unayoomba.Kumbuka mara baada ya kupata fursa ndipo mtakapojadili suala la mshahara nawewe utaona kama kiwango kinafaa.

2.Ni lini kiwango cha mshahara wangu kitapanda?Hili swali ni baya pengine kuliko la kwanza.Kuhusu kupanda kwa mshahara inategemea baadhi ya  mashirika yako na utaratibu wa wazi lakini mengine hayako hivyo,jambo la msingi niwewe kufanya utafiti wa kina pindi unapopata kazi husika.Zingatia kwamba wakati wa usaili wewe unatakiwa kuangalia suala la kutetea nafasi uloomba sio kuchunguza maslahi.

3. Je utaratibu wa likizo ukoje katika shirika hili? Swali hili ukiliuliza ni wazi kwamba uanonesha kuwa hujafanya utafiti wa kutosha kuhusu shirika,lakini jambo la kuzingatia hapa ni kwamba suala la likizo mara nyingi ni taarifa ambazo si za siri ni wajibu wako kufuatilia kwa kina kabla hata hujaomba kazi ili upate kujua wakati mwingine huwekwa hata kwenye mtandao wa shirika.
   
………..Maktaba YETU leo……….


 . “Never hire someone who knows less than you do about what he’s hired to do.”
              Malcolm ForbesForbes
Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi