Si kwamba wanaokoswa ajira baada ya
usahili(interview) hawana majibu sahihi.Hili si kweli ukweli uliopo ni kuwa mtu
anaingia kwenye usahili pasipo kujua ni namna gani anaweza kujibu maswali hivyo
huishia kukoswa ajira ambayo ilikuwa ni stahiki yake kabisa. Haya hapa ni mambo
matatu ya kuzingatia wakati unapoingia katika chumba cha usahili na kuanza
kujibu maswali hakika ikiyazingatia wewe hautakuwa wa kushindwa usahili kila
mara.
Zungumza taratibu na
kwa uhakika.( speak slowly and clearly)
Unapojibu swali inakupasa ujibu kwa
sauti ya kawaida na kwa uhakika hii itaonesha ni jinsi gani unaelewa kile
unachosema.Pia unapoongea kwa taratibu itakuwa rahisi kwako kuweza kupangilia
mawazo yako vema.Wengi wamekoswa ajira kwa sababu ya kuongea kwa haraka na
kupelekea kushindwa kueleweka wanachosema.
Weka kituo kabla hujaanza kujibu swali.(Pause slightly before you begin)
Unapoulizwa swali hakiksha unafikiria
kabla ya kujibu hili uwe na majibu sahihi.Sina maana ukae muda mrefu unafikiria
jibu hii nayo si nzuri,hapa cha kuzingatia ni kuwa na mwanzo mzuri wa kujibu
wenye tafakari ya uhakika kuliko kujibu wakati hata hujui unajibu nini
Andaa majibu kwa
baadhi ya maswali ya msingi(Prepare answers
to some basic questions)
Maswali ya msingi hutokana na jinsi nafasi
unayoomba hivyo ni vizuri ukawa na majibu hayo mapema ili unapoulizwa usitumie
muda mwingi kufikiria,pia utajibu kwa uhakika kwa sababu majibu umeyazoea
tayari.Kumbuka kuwa makini na kile ulichoandika katika barua yako ya maombi na
taarifa za kwenye “CV” yako.Wengi wamekoswa ajira kwa kuandika vitu katika “CV”
zao na wanashindwa kuvieleza.
………..Maktaba YETU leo……….
“Never hire someone who knows less than you do about what he’s hired to do.”
“Never hire someone who knows less than you do about what he’s hired to do.”
– Malcolm Forbes, Forbes
Post a Comment