Home » » Haya ndo maandalizi ya awali katika usaili-1

Haya ndo maandalizi ya awali katika usaili-1

Written By Unknown on Sunday, November 30, 2014 | 11:51 AM


JITAMBUE
Hatua ya kwanza kabla ya kufanya usaili ni vizuri ukajifanyia tathmini wewe binafsi ili utambue  kitu gani unaweza kufanya kwa mwajiri iwapo utapata fursa.Ni vema ukajitathmini kwa kuzingatia ujuzi na udhoefu ulonao ambao utakufanya kujiuza zaidi kwa mwajiri wako wakati wote wa usaili.Jambo la muhimu katika kujiuza kwa mwajiri anza na uzoefu wako katika kazi kwa kutaja na kuelezea kwa undani shughuli ambazo umekuwa ukizifanya ( Katika ajira ya awali,Kazi za kujitolea,Miradi shuleni n.k) Kumbuka katika yote hayo usihanisha na nafasi unayoomba.

ANDAA MAVAZI UTAKOYOVAA KATIKA USAILI.
Kile utachovaa katika usaili pia ni sehemu muhimu sana katika maandalizi ya usaili.Ukishatambua nini utavaa katika usaili siku moja kabla ya usaili ni jambo jema sana kwani utapata fursa ya kujiandaa katika maeneo mengine ambayo yanahitaji utulivu wa kiakili zaidi.Hivyo unashauriwa kulifanya suala la mavazi mapema kuliko kusubiri siku ya usaili laweza kukupotezea muda mwingi sana.

SOMA WASIFU WAKO (CV) NA KUELEWA KILA KITU
Kila kitu ulichoandika katika “CV” yako kinaweza kujadiliwa katika usaili,kwa kuwa mwajiri huisoma “CV” yako na kukufahamu wewe na ndipo hufanya maamuzi ya kukuita katka usaili.Hivyo mwajiri anaweza kuchagua kipengele kimojawapo katika “CV” yako na kukutaka utoe ufafanuzi hata kama ni kazi ulofanya kwa kipindi kirefu kilichopita utatakiwa kukitolea ufafanuzi wa kina.Hivyo zingatia kusoma “CV” yako kwa umakini na kuelewa kila kipengele katika “CV” yako.
Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi