Home » , , » Mambo manne ambayo makampuni ya kibiashara huyatarajia katika CV yako.

Mambo manne ambayo makampuni ya kibiashara huyatarajia katika CV yako.

Written By Unknown on Monday, March 2, 2015 | 1:41 PM




Ni wazi kuwa katika biashara kila kampuni au taasisi huwana malengo yake ambayo hutaraji kuyafikia katika kipindi fulani.Mara nyingi malengo hayo hufikiwa kwa kupitia watumishi wa kampuni husika.Baada ya utafiti wa muda mrefu imegundulika kuwa makampuni ya kibiashara huhitaji watu wenye sifa kuuu nne.Hivyo unapoandika CV yako zingatia mambo haya ya msingi.
Ni kwa vipi unaweza kukuza biashara,mfanyabiashara mara zote hupenda kuona biashara yake ikikuwa,hivyo kama umewahi kufanyakazi kwenye kampuni ya kibiashara na unaomba kazi onesha ni kwa vipi ulitoa mchango wako katika kukuza biashara ile,Kama wewe hujawahi kufanya kazi onesha ni kwa vipi unaweza kuchangia katika kukuza biashara na kampuni kwa ujumla.
Ni kwa vipi unaweza kutengeneza faida,hakuna biashara isiyohitaji faida ili iweze kujiendesha Hivyo mwajiri hupenda kuona ni kwa vipi mtumishi anavyoweza kukabiliana na soko na kuleta faida katika kampuni kwa njia mbalimbali.Hivyo katika CV yako zingatia sana jambo hilo unapoandika
Ni kwa vipi unaweza kukuza soko la biashara,Ukuzaji  wa soko mara nyingi umekuwa na tija kwa makampuni kwani huweza kuwafikia wateja wengi  na kuuza bidhaa husika kwa wingi.Hivyo jambo la kuzingatia kwa mwajiri unapoomba kazi anaangalia udhoefu wako au mbinu ulizonazo zinazoweza kusaidia katika kukukuza soko.
Ni kwa vipi unawezakusaidia utengenezaji wa bidhaa mpya.Katika biashara mabadiliko ni muhimu kutokana na sabababu mbalimbali,hivyo mwajiri yoyote hupenda kuona mtumishi anayeweza kuleta mabadiliko katika bidhaa,Unapoandika CV zingatia sana kipengele hiki.
Kumbuka unapoandika CV onesha mambo ulofanikwa kuyafanya yenyeuhusiano wamoja kwa moja na kazi husika ondoa mambo yote yasiyo ya lazima katika nafasi husika.


Share this article :

Post a Comment

 
Owner : Amewezaje team | Join us on Facebook | Welcome again
Copyright © 2015. Amewezaje - All Rights Reserved
Designed by Kijiwe Cha Wasomi